Tuesday, November 15, 2016

1FMTZ: breaking news Mshambuliaji wa Hull City kutocheza kwa mwaka mmoja


Mshambuliaji wa Hull City, Will Keane hatocheza soka kwa miezi 12 kutokana na jeraha la goti.
Keane , 23, alipata jeraha hilo katika mechi dhidi ya Southampton ambayo walipata ushindi wa mabao 2-1 na atafanyiwa upasuaji siku ya Jumanne.

Mshambuliaji huyo aliejiunga na Hull City kutoka Manchester United tarehe 30 mwezi Agosti ameshiriki mechi 6 kwa upande wa Mike Phelan.
''Kumpoteza mchezaji wenye kiwango kama cha Will kwa muda mrefu ni pigo kubwa '', Phelan ameiambia tovuti ya klabu hiyo.
Hull, kwa hivi sasa iko katika nafasi ya 18 katika ligi ya premia , pointi moja nyuma ya WestHam

No comments:

Post a Comment

Disqus Shortname

Comments system