Siku zimepita na miaka imekwenda hakuna kolabo tuliyoiona lakini “ukistaajabu ya Mussa utayaona ya Firauni,” ndio tuliyoyaona. Ndipo nikaukumbuka wimbo malkia wa muziki wa Bongo Fleva, Lady Jaydee ‘Siku Hazigandi’ baada ya kuona urafiki uliogeuka undugu wa damu ukiteketea na kugeuka majivu baada ya kuunguzwa na mwanga wa tochi – ni kitu cha kushangaza na kisichowezekana lakini kwa hapo kiliwezekana.
Nilifurahi sana kuna busara iliyotumika kwa kila mmoja kukaa kimya bila ya kumshtumu mwenzake kwa lolote na kila mmoja akifanya kazi kivyake lakini ghafla nuru ya mwanga uliopo kugeuka giza baada ya usiku wa Jumanne hii mtandao wa Instagram ukigeuka uwanja wa ‘Kitchen Party’ kwa Ommy na Diamond kutupiana vijembe vya maneno ya kashfa na kuanza kutoleana siri ambazo kwa mashabiki hatuna uhakika nazo labda wao wenyewe wanajua juu ya ukweli wausemao kwa jamii.
Diamond alianza kwa kuandika kwenye kipande cha video ya wimbo mpya wa Rich Mavoko aliyoiweka kwenye mtandao huo, “Kushindana na Wasio Jua Raha sana hahahahahaha 


…….”
Ommy Dimpoz alijibu kwa kuandika:
Wazee Wa Kupanik Mbona Kama Povuuu Linawatoka #TeamMzikiMzuri VS #TeamUjanjaUjanja
#Kajiandae
#KabaliYao
#WeDontBuyViews
#MeNilijuaTunafanyaMzikiKumbeVitaaa
#NawajuaWazeeWaKuchambaNataniaTu
#PiaNawajuaKwaMitusiLakiniNishajiandaa
#NawaachiaUwanjaMweupeeeWalaSiblokuMtu
#NachangamshaBarazaKidogoooo
#Kajiandae
#KabaliYao
#WeDontBuyViews
#MeNilijuaTunafanyaMzikiKumbeVitaaa
#NawajuaWazeeWaKuchambaNataniaTu
#PiaNawajuaKwaMitusiLakiniNishajiandaa
#NawaachiaUwanjaMweupeeeWalaSiblokuMtu
#NachangamshaBarazaKidogoooo
Diamond alishindwa kuvumilia naye aliandika, “Mtoto wa Kiume kumchukia Mwanaume Mwenzio kisa Kakataa kukupumulia nayo ni #KOKORO.”
Kwa watu wanaofahamu zaidi maneno ya mitaani wanaweza kufahamu kilichoandikwa ndani kina maana gani tena hayapaswi kuandikwa na wasanii wakubwa kama hawa kwenye hadhira hii. Wakati huo huo siku hizi mitandao ya kijamii inatembelewa mpaka na watoto wadogo, je watoto wao au hata ndugu zao wadogo wanaowalea na kuwategemea wakiona mtu anayemuheshimu nyumbani amefanya hivyo mitandaoni unafikiri itakuwaje?
Kumbukeni mlipotoka kwa kuwa ‘Adui yako wa leo ndio rafiki yako wa kesho, na rafiki yako wa leo ndio adui yako wa kesho’.
No comments:
Post a Comment